Monday, November 23, 2009

Vipaji lukuki....


Producer Vin

Fredyrasta
Mysore imekuwa na historia ndefu kwa Watanzania tangia miaka 60 wamekuwa wakija kupata elimu na kuondoka, miaka ya karibuni tuliona Vipaji vya hali ya juu kutoka kwenye soka ya miguu mpaka,mpira wa Kikapu.

Vipaji vya mpira vilivyoonekana wakati huo kutoka kwa akina Saphy's(Salehe na Hussein)ni moja ya changa moto tosha ,pia kwenye mpira wa Kikapu Baraka Matawalo anastahili sifa.

Wajasiliamali nao hawakuwa nyuma wengi waliomaliza hapa 1997 na 2001 wametoa changamoto ambazo zinaonekana wazi na kwa waliomaliza 2007,mfano Kijana Wanda ama Steven Mzaba na Joshua Kazi 2009 ambao wamejikita kweli kweli kwenye ujasiliamali.

Leo katika wimbi la vipaji basi tuwaone vijana watatu katika swala zima la Burudani,Producer Vin,Man Kim na Fredy rasta ,pitisha wacho kwenye blog hii utapata habari zao wassapebongoproduction.blogspot.com

Friday, November 20, 2009

Mambo ya madiko diko ya kinyumbani....



Uwanja wa ubunifu na mambo ya Ujasiliamali yamezidi kupambazuka hapa mjini Mysore,Wadada wawili wamekuja kivyao na kuanzisha kitu kizuri, wadada hao ambao wameamua kutoa huduma ya Chakula chenye ladha ile ile ya Nyumbani.Tafadhali watembelee hapa..www.hotchicken65.blogspot.com hapa unaweza kupata taarifa zao,tujumuike pamoja as Mysore One'the Movement' katika kudumisha umoja.

Wednesday, November 18, 2009

Good Times....

Sauti za Busara 2010

SLAVE TO THE RHYTHM


http://www.reelbrazil.co.nz/times/Slave_to_the_rhythm.html

Sunday, November 15, 2009

Register now for a special public speaking Training Program.

Wednesday, November 11, 2009

Kilimanjaro Acrobatic Group ilivyotesa Mysore....


Kaka wanaofanya kazi ya ziada...

Wadada wanaojituma kazini wakiwa kwenye picha ya pamoja.

Kila mtu kapewa kipaji chake.....hapa vija wakionyesha uwezo wa juu katika sarakasi.

Burudani kutoka kwa viajan wa Kitanzania.

Wasanii wa Kilimanjaro Acrobatic Group wakiwa kazini mjini Mysore...

Vijana 8 wa Kitanzania walifanya maonyesho kadhaa ya sarakasi wakishirikiana na Gemini Circus walionyesha show mbali mbali za sarakasi,vijana hao ambao kwa pamoja waliweza kuonyesha maajabu na uwezo wa juu katika sarakasi...pia kwa pamoja wameshukuru sana Watanzania wenzao wa Mysore kwa kutoa ushirikiano wa bega kwa bega ambao ulichangia kuonyesha ufanisi wa hali ya juu,wakiwa wanatokea Kikundi kijulikanacho kama Kilimanjaro Acrobatic Group, vijana hao nane sasa wameelekea mji wa Mandya kisha watamalizia ziara yao mjini Bangalore....